Trending News

CCM Adverts and Promo

Monday, March 21, 2016

DKT. SHEIN AIBUKA MSHINDI KITI CHA URAIS ZANZIBAR, APATA ASILIMIA 91.4

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar  ZEC  Jecha Salim Jecha amemtangaza Dk Ali Mohamed Shein kuwa mshindi wa kiti cha urais visiwani humo baada ya kupata kura 299.982 sawa na asilimia 91.4 ya kura zote zilizopigwa  ambapo chama cha wananchi CUF kilitangaza kususia huku vyama vingine vikishiriki.

Uchaguzi wa Zanzibar ulifutwa  Oktoba 25 mwaka jana baada ya dosari mbalimbali kujitokeza ikiwemo ya aliyekuwa mgombea wa urais kupitia chama cha CUF Maalim Seif Sharif Hamad kujitangazia ushindi jambo lililopelekea  Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha kutangaza kuufuta uchaguzi huo.

No comments:

Post a Comment