Mwenyekiti
wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC Jecha Salim Jecha amemtangaza
Dk Ali Mohamed Shein kuwa mshindi wa kiti cha urais visiwani humo baada ya kupata kura 299.982
sawa na asilimia 91.4 ya kura zote zilizopigwa ambapo chama cha wananchi
CUF kilitangaza kususia huku vyama vingine vikishiriki.
Uchaguzi
wa Zanzibar ulifutwa Oktoba 25 mwaka jana baada ya dosari mbalimbali
kujitokeza ikiwemo ya aliyekuwa mgombea wa urais kupitia chama cha CUF Maalim Seif
Sharif Hamad kujitangazia ushindi jambo lililopelekea Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha kutangaza kuufuta uchaguzi
huo.


No comments:
Post a Comment