Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga Abdul
Rashid Dachi akikabidhi chakula kwa Wazee wa kituo cha Kolandoto Mkoani Shinyanga kwa niaba
ya Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli ametoa chakula kwa Wazee wanaoishi katika
kituo cha Wazee cha Kolandoto
kilichopo Manispaa ya Shinyanga Mkoani
Shinyanga kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
Akikabidhi chakula hicho kwa niaba ya
Mhe. Rais, Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bw. Abdul Rashid Dachi,
amewaeleza wazee hao kuwa Mhe. Rais anawatakia kila la heri katika Sikukuu
ya Pasaka na ameahidi atakapopata nafasi atawatembelea kituoni hapo.
Naye Mwenyekiti wa Wazee hao Mzee
Samwel Maganga amemshukuru sana Mhe.Rais kwa kuwakumbuka na kuwajali
katika sikukuu hiyo.
Na. Magdalena Nkulu
Ofisi
ya Mkuu wa Mkoa
Shinyanga


No comments:
Post a Comment