Chama cha mapinduzi (CCM)
kimemteua Mbunge wa Zamani wa SIMANJIRO mkoani Manyara, CHRISTOPHER OLE SENDEKA
kuwa msemaji wa chama hicho.
Akitangaza hatua hiyo
katika mkutano na waandishi wa habari Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM,
Lumumba jijini Dar es Salaam jijini DSM
Katibu mkuu wa CCM ABDULRAHMAN KINANA amesema uteuzi wa OLE SENDEKA kuwa msemaji
wa chama hicho, ni hatua ya kupunguza majukumu ya kiutendaji kwa aliyekuwa
msemaji wa chama hicho NAPE NNAUYE aliyeteuliwa kuwa waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Kinana amesema hatua
hiyo itatoa fursa kwa watendaji hao kutimiza majukumu yao kwa ufanisi zaidi
katika kuwatumikia wananchi.
Akizungumza mara baada
ya uteuzi huo,msemaji huyo wa CCM CHRISTOPHER OLE SENDEKA ametoa wito kwa
wanasiasa nchini kuacha siasa za kuponda jitihada mbalimbali
zinazochukuliwa na serikali ya awamu ya tano katika kutimiza majukumu yake,
ambapo amesema hatua hiyo ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama cha
mapinduzi.

No comments:
Post a Comment