Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Malinyi ndugu Fadhili Liguguda akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Wazazi Mkoa wa Morogoro Bi. Mecktridis Mdaku.
Mwenyekiti wa
Wazazi Mkoa wa Morogoro Bi. Mecktridis Mdaku ametoa msaada wa mahindi kwa
wananchi walioathiriwa na mafuriko katika maeneo ya Malinyi, Usangule na Itete.
Akikabidhi
msaada huo kwa niaba ya Bi. Mdaku, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya
Malinyi ndugu Fadhili Liguguda amesema kuwa, Msaada huo uliogharimu shilingi
milioni moja(1,000,000/=) umekabidhiwa kwa wananchi wa maeneo husika.
Ndugu
Liguguda, amewaomba wananchi hao kutumia msaada huo kwa malengo yaliyokusudiwa. Aidha, wananchi hao kuendelea na kilimo kwani bila kilimo watakumbwa na
baa la njaa.
Amemshukuru Bi. Mdaku kwa msaada alioutoa na aendeelee kuwa na moyo kama huo wa upendo na
unyenyekevu kwa wananchi wowote wanaokumbwa na majanga kama hayo.
Kwa upande wao wananchi wa Itete, Usangule na Malinyi wamemshukuru mwenyekiti wa Wazazi Mkoa
wa Morogoro bibi. Mecktridis F.Mdaku kwa msaada aliowapatia. Wamemuomba azidi
kushirikiana nao katika majukumu ya kujenga Taifa letu.


No comments:
Post a Comment