Trending News

CCM Adverts and Promo

Thursday, April 7, 2016

WANANCHI WA MALINYI MKOANI MOROGORO WAPATA BOT

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya  ya Malinyi ndugu Fadhili Liguguda akizindua boti itakayofanya kazi ya usafirishaji wa abiria katika mto Mnyera uliopo Malinyi mkoani Morogoro.
Baadhi ya wananchi wakishuhuhudia  boti hiyo ikiingizwa mto Mnyera uliopo Malinyi mkoani Morogoro.


Boti hiyo ikianza kazi ya kuvusha watu ndani ya mto Mnyera 
 
Na. Mwandishi Wetu - Morogoro.
 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya  ya Malinyi ndugu Fadhili Liguguda amezindua boti itakayofanya kazi ya usafirishaji katika mto Mnyera uliopo Malinyi mkoani Morogoro.

Akizindua chombo hicho cha usafirishaji amesema kuwa Boti hiyo itarahisisha utendaji wa kazi husususan wananchi kuwezeshwa kuvuka kutoka eneo moja la mto hadi lingine kwa urahisi zaidi tofauti na awali ambapo walikuwa wakipata shida wakati kipindi cha mvua.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Malinyi ndugu Said Msolmoka akizungumza wakati wa makabidhiano kivuko hicho amesema kuwa kimegharimu fedha za kitanzania shilingi milioni tisa(9,000,000/=).

Ndugu Msomoka amewaomba wananchi na wahusika wanaoisimamia boti hiyo kuitumia kwa uangalifu na kwa malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wao wananchi wa Malinyi wameishukuru halmashauri hiyo kwa msaada huo ilioutoa wakieleza kuwa hapo awali maisha yao yalikuwa hatarini kwa kuliwa na mamba kutokana na kukosekana kwa usafiri wa uhakika.

Wananchi hao wamemuahidi mkurugenzi huyo kuwa watakitunza chombo hicho na kukitumia kwa kazi iliyokusudiwa.

Katika hatua nyingine uongozi wa wilaya ya Malinyi umetembelea Hospitali ya Lugalo iliyomo Malinyi na kupanda miti 1500  na kufanya usafi wa mazingira.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa zoezi la kufanya usafi wa mazingira na kupanda miti Mkurugenzi wa wilaya hiyo ndugu Said Msolomoka, amesema Wilaya yake inamuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli katika suala la usafi.

Amesema kama Halmashauri ya wilaya wametenga siku maalum kila mwanzo wa mwezi kwa ajili  usafi.

No comments:

Post a Comment