Trending News

CCM Adverts and Promo

Sunday, May 22, 2016

MEJA JENERALI JAMES MWAKIBOLWA ATUNUKIWA NISHANI YA ULIPUAJI BORA WA MIZINGA

Meja Jenerali James Mwakibolwa.
 
 ********************************************************
Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Marekani linaloshughulikia masuala ya kijeshi barani Afrika, Meja Jenerali Darrly Williams, amemtunuku mkuu wa majeshi ya vikosi vya nchi kavu Tanzania Meja Jenerali James Mwakibolwa nishani ya ulipuaji bora wa mizinga nchini.

Nishani hiyo ambayo imekuwa ikitolewa na Rais wa Marekani, alitunukiwa Meja Jenerali Mwakibolwa baada ya kuwa mstari wa mbele kurudisha amani kwenye nchi zinazokabiliwa na vita barani Afrika.

Akizungumza wakati wa kufunga mkutano wa wakuu makamandi wa vikosi vya nchi kavu barani Afrika, uliofanyika mkoani Arusha, Jenerali Williams alisema jeshi la Marekani barani Afrika, linamtambua Mwakibolwa kuwa mchapa kazi bora.

“Mwakibolwa ni mtaalamu sana kwenye masuala ya mizinga, hata tulipokwenda kwenye mafunzo ya kijeshi katika kambi ya Monduli, tumeona umahiri wake na tuzo hii anastahili kwa kuwa anafanya vizuri.

“Jeshi la Tanzania limekuwa mstari wa mbele kutoa kikundi cha M23 kwenye nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na yote hayo ni kutokana na uchapakazi wa Jenerali Mwakibolwa,” alisema Jenerali Williams.

Akitoa maoni yake kuhusu tuzo hiyo, Jenerali Mwakibolwa aliahidi kuhakikisha Jeshi la Tanzania linakuwa imara zadi barani Afrika.

No comments:

Post a Comment