Trending News

CCM Adverts and Promo

Tuesday, May 10, 2016

TASWIRA ZA MWENYEKITI WA CCM TAIFA NA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA NNE DKT.JAKAYA KIKWETE KWENYE DARAJA LA NYERERE JIJINI DAR ES SALAAM


Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Uchukuzi Mhandisi Joseph Nyamhanga mara baada ya kuwasili katika daraja la Nyerere lililopo Kigamboni.

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete(wa pili kulia) akipokea maelekezo kutoka kwa kwa Meneja Mradi wa daraja la Nyerere Mhandisi Karim Mattaka wakati alipotembelea daraja la Nyerere lililopo kigamboni.

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete( wa pili kushoto) akiangalia uzuri wa daraja la Nyerere leo Jijini Dar es Salaam alipotembelea daraja hilo Kulia ni Mke wa Rais Mstaafu Mama Salma Kikwete , wa pili kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Uchukuzi Mhandisi Joseph Nyamhanga na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke  Sophia Mjema.

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete( wa pili kushoto) akimsikiliza mkewe mama Salma Kikwete (wa pili kulia) wakati alipotembelea daraja la Nyerere lililopo kigamboni katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Uchukuzi Mhandisi Joseph Nyamhanga, kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Temeke  Sophia Mjema.

Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete(kushoto)  akisikiliza maelezo juu ya ukusanyaji wa mapato katika daraja la Nyerere kutoka kwa msimamizi mkuu wa ukusanyaji mapato Bw. Gerald Sondo.Picha/Raymond Mushumbusi

No comments:

Post a Comment