|
Wabunge wakifurahia mara baada ya kupitisha Bajeti ya Serikali kwa
mwaka wa fedha 2016/2017.
|
|
Waziri wa fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango watano kutoka
kushoto akiwa na baadhi ya watendaji wa Wizara ya fedha na Mipango nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya
kupitishwa kwa bajeti Kuu ya Serikali, leo mjini Dodoma.
|
(Picha na Frank Mvungi)
Na: Lilian Lundo – DODOMA
Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo limepitisha
bajeti ya shilingi Trilioni 29.5 ya mwaka wa fedha 2016/17 ambayo iliwasilishwa
na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango June 08, 2016.
Bajeti hiyo ilipigiwa kura na wabunge waliokuwepo bungeni,
ambapo jumla ya wabunge 251 walipiga kura za ndio za kuipitisha bajeti hiyo
kati ya wabunge 252 waliokuwepo ukumbini wakati
kura hizo zikipigwa.
Katika kupiga kura Hakukuwa na kura yoyote ya hapana au
kutokuamua kati ya wabunge waliopiga kura. Jumla ya wabunge 137 hawakuwepo
wakati kura zinapigwa.
“Naipongeza Serikali
kwa kutoa hoja ya bajeti ya Serikali ya mwaka 2016/17 na kupitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
namtakia Waziri wa Fedha kila la heri katika hatua zinazofuata katika
utekelezaji wa bajezi hii,” alisema Naibu Spika Mhe. Dkt. Tulia Ackson.
Aidha bunge hilo, lilipitisha muswada wa sheria za Serikali
kuidhinisha Trilioni 29.5 kwa matumizi ya Serikali kutoka mfuko wa hazina kwa
mwaka unaoishia June 30, 2016.
Kwa upande wake, Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip
Mpango amewataka watanzania kulipa kodi
na wale wote wanaotakiwa kusimamia ukusanyaji wa kufanya kazi hiyo kwa
ukamilifu ili fedha zilizopitishwa katika bajeti ya mwaka 2016/17.
Sheria hiyo ya bajeti ya mwaka 2016/17 inasubiri kusainiwa na
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo
utekelezaji wake utaanza Julai 01, 2017.
No comments:
Post a Comment