Umoja wa
Wazazi Tanzania kila mwaka huadhimisha wiki ya Wazazi ambayo huadhimishwa
kuanzia tarehe 1-6 April kila Mwaka.
Kitaifa
Mwaka 2014 maadhimisho hayo yaliadhimishwa Kisiwani Pemba, ambapo mgeni rasmi
alikuwa Mwenyekiti wa Wazazi Taifa Alhaj Abdalah Majura Bulembo (MCC). Na kila
Mkoa waliadhimisha wiki hiyo katika mikoa yao Kwa kufanya shughuli mbalimbali
za Kijamii ikiwemo Usafi wa Mazingira, upandaji miti na kutembelea watoto
yatima na waathirika wa HIV na madawa ya kulevya.
Mkoa wa
Morogoro waliadhimisha wiki ya Wazazi katika Wilaya ya Mvomero ambapo Makatibu na Wenyeviti wa Wilaya zote
za Mkoa huo walihudhuria.


No comments:
Post a Comment