Wajumbe wa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, wakikagua Kiwanda cha kuchakata gesi
asilia cha Madimba mkoani Mtwara,
Baadhi ya wataalam
kutoka Wizara ya Nishati na Madini, wakijadiliana jambo wakati wa ziara ya
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini katika Kiwanda cha kuchakata
gesi asilia cha Madimba mkoani Mtwara hivi karibuni. Kutoka kushoto ni Afisa wa
Bunge Amon Marco, Mhandisi Godson Chacha, Afisa wa Bunge Msaidizi (Madini) Andendekisye
Mbije, Afisa wa Bunge Msaidizi (Nishati) Kalory Mmasy na Mhandisi Robert Dulle.
Meneja Mkuu Kampuni
ya Kusambaza Gesi (GASCO), Mhandisi Kapuulya Musomba (wa pili kushoto),
akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini,
walipokuwa katika ziara kukagua Mradi huo mkoani Mtwara hivi karibuni.
Naibu Waziri wa
Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha
Msimbati, alipokuwa katika ziara pamoja na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati
na Madini, kukagua Mradi wa Bomba la Gesi.




No comments:
Post a Comment