Trending News

CCM Adverts and Promo

Thursday, April 14, 2016

WAZIRI WA TAMISEMI MHE. SIMBACHAWENE AIVUNJA BODI YA USIMAMIZI WA JENGO LA MACHINGA COMPLEX LA DAR ES SALAAM

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Mhe.George Simbachawene(wa pili kulia) akiimba wimbo wa taifa pamoja na wageni wa meza kuu wakati wa  ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) jijini Dar es Salaam

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Mhe.George Simbachawene (Katikati) akiingia ukumbi wa Diamond jubilee jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) ambapo walizungumzia changamoto mbalimbali zinazowakabili, kulia kwake ni  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Raymond Mushi.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Mhe.George Simbachawene(wa pili kulia) akiwa katika meza kuu baada ya kuingia ukumbi wa Diamond jubilee jijini Dar es Salaam ukumbuni kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), kulia kwake ni  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Raymond Mushi Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Bw.Johnson Minja  .



Wanachama wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) kutoka mikoa mbalimbali nchini wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa Jumuiya hiyo ulifanyika jijini Dar es Salaam.

Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya Ya Wafanyabiashara Tanzania Bw.Jeda Hasaan akiongea wakati wa Mkutano wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania,uliokuwa ukijadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara,leo jijini Dar es Salaam.


Mwenyekiti wa Jumuiya Ya Wafanyabiashara Tanzania Bw.Johnson Minja akisoma risala wakati wa Mkutano wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania,uliokuwa ukijadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara,leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akiongea na wanachama wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania wakati wa  mkutano mkuu wa jumuiya hiyo ,uliokuwa ukijadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara,leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Mhe.George Simbachawene akitoa risala wakati wa  ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) ambapo walizungumzia changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Mhe.George Simbachawene (wa pili kushoto) akiwa katika Picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa  Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) uliofanyika leo jijini Dar es salaam uliokuwa ukizungumzia changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara.(Picha na Lorietha Lawrence)


(Na Lorietha Laurence- Dar es salaam).
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Mhe.George Simbachawene ameifuta Bodi ya usimamizi wa jengo la Machinga Complex la jijini Dar es salaam na kumuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda kulisimamia kwa kuhakikisha kuwa  linatumiwa na wafanyabiashara wadogo wasiokuwa na maeneo maalum ya kufanyia biashara.


Ametoa agizo hilo Leo jijini Dar es salaam mara baada ya kupokea changamoto zinazowakabili wafanyabiashara  wa jiji hilo wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa  Jumuiya ya wafanyabishara Tanzania(JWT).

“Naomba Mkuu wa mkoa usimamie jengo hili kwa kuhakikisha wale wafanyabiashara wadogowadogo waliopo pembezoni mwa barabara maeneo ya karume na wengine wasio na sehemu za kufanyia kazi kufanya biashara zao hapo” alisema Mhe Simbachawene


Amesema wafanyabishara hao wanatakiwa kunufaika kwa kupatiwa maeneo maalum ya kufanyia kazi huku akieleza kuwa ni wajibu wa serikali kuhakikisha inatenga maeneo hayo ikiwemo machinga complex ambayo ipo kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo wadogo.


Amewataka Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kuwa walezi wa Jumuiya za Wafanyabiashara katika mikoa na wilaya zao ili kupata nafasi ya kukaa pamoja na  kujadili matatizo mbalimbali yanayowakabili na  namna ya kuyatatua.


Pia ameziagiza Halmashauri  kutokutumia nguvu  katika kukusanya kodi bali washirikiane na wafanyabiashara ikiwemo kuwapatia  elimu ya umuhimuwa ulipaji kodi ili kuwepo na uwazi na uwajibikaji kati ya pande zote mbili.



“Naomba tuondokane na dhana ya mgambo kunyang’anya wafanyabiashara bidhaa zao na badala yake uwekwe utaratibu wa  kuwapatia elimu ya mlipa kodi ili waweze kutambua umuhimu wa kulipa kodi kwa hiyari kwa maendeleo ya Taifa ” alisema Mhe.Simbachawene.


Waziri Mhe.Simbachawene pia ameahidi kusimamia uwazi na uajibikaji katika ulipaji kodi kwa kuhakikisha kuwa  sheria na taratibu za ulipaji kodi zinafuatwa na kuzingatiwa na hivyo kuondokana na kodi elekezi ambazo zinapelekea  mianya ya rushwa kwa watendaji wa serikali na wafanyabiashara na hivyo kuliletea taifa hasara.


Aidha amesema kuwa atayasimamia mapendekezo yaliyotolewa na Jumuiya hiyo ya Wafanyabiashara ikiwemo uwazi na uwajibikaji katika ulipaji wa kodi bandarini ,utoaji wa lesini uwe kwa kipindi cha miaka mitano au mitatu na udhibiti wa utoaji holela wa lesini za biashara kwa wafanyabiashara wageni.


Kwa Upande wa Mwenyekiti wa Jumuiya Ya Wafanyabiashara Tanzania Bw.Johnson Minja ametoa wito kwa serikali kuboresha mazingira ya wafanyabiashara ili kuwa na walipa kodi halali watakaokuza uchumi wa nchi kutoka uchumi wa kati hadi uchumi wa viwanda na hivyo kukuza pato la taifa.


No comments:

Post a Comment