Trending News

CCM Adverts and Promo

Wednesday, May 4, 2016

MARUFUKU KUTOZA USHURU WA MAZAO MAGETINI.

Katika kutekeleza ahadi ya kuboresha maisha na vipato vya wakulima kote nchini Serikali imeondoa ushuru wa mazao uliokua unatozwa  kwenye mageti na kufafanua kuwa ushuru huo sasa utatozwa mazao yanapofika sokoni tu.

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Nchemba amelieleza Bunge mjini Dodoma akifafanua kuwa kwa kipindi kirefu mazao ya wakulima  yamekuwa yakitozwa ushuru yanapofika mipaka ya kata kwenye mageti maalumu na hata yanaporudishwa mashambani, hali ambayo imekuwa ikilalamikiwa sana na wakulima nchini.

 Akiwasirisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017 bungeni Dodoma Katika mwaka ujao wa fedha amesema  wizara hiyo imeomba kuidhinishiwa Sh 275,063,518,000. 

. Mhe. Mwigulu ametangaza neema kwa wakulima kwa kuwaambia kuwa pembejeo za kilimo sasa zitapatikana kwa wingi.
Amesem wizara inapitia upya mfumo wa sasa wa vocha za pembejeo kwa lengo la kupata mfumo utakaowezesha upatikanaji wa mbolaea kwa wakulima wote wanaohitaji kupitia maduka ya pembejeo kwa bei nafuu.

No comments:

Post a Comment