 |
| Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akiongea wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa
wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao ambapo pamoja na
kuishukuru ofisi ya Bunge kwa kazi hiyo pia ameahidi serikali yake kuendelea
kukabiliana na changamoto zilizokatika sekta ya elimu ikiwemo upungufu wa
vyumba vya madarasa ili kuwawezesha wanafunzi kuwa na mazingira rafiki ya
kujifunzia. Leo katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam. |
 |
| Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. Tulia Ackson akiongea wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa
waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao ambapo alisema
ofisi ya bunge inatarajia kugawa jumla ya madawati 61,385 katika majimbo 155
kati ya majimbo 264 ambapo ni sawa na asilimia 59 wa madawati 120,000
yanayotarajiwa kutengenezwa na ofisi hiyo Leo katika viwanja vya Karemjee
Jijini Dar es Salaam. |
 |
Meya wa Jiji la Dar
es Salaam Mstahiki Meya Isaya Mwita akiongea wakati wa hafla ya utoaji madawati
kwa waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao na
kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa
jitihada zake za kukabiliana na changamoto katika sekta ya elimu nchini.
|
 |
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na baadhi ya
watoto wa shule ya msingi Bunge wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa
waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao, Leo katika
viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam.
|
 |
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua madawati katika mfano wa
Darasa wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa ajili ya
shule zilizo kwenye majimbo yao, katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar es
Salaam. Anayemfuata ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.
Kassim Majaliwa na kulia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. Tulia Ackson.
|
 |
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Mbunge wa Jimbo la
Ilala Mh. Idd Azzan Madawati yaliyotolewa na Ofisi ya bunge kwa ajili kwa niaba
ya wabunge waliopata mgao huo katika awamu ya kwanza.Wanaoshuhudia kutoka
kushoto ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia
Ackson, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa
waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao, katika
viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam.
|
 |
| Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waheshimiwa
wabunge waliohudhuria hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa
ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar
es Salaam. |
 |
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na
wanafunzi kutoka shule ya msingi Bunge iliyopo Jijini Dar es Salaam, wakati wa
hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa ajili ya shule zilizo
kwenye majimbo yao katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar es Salaam.
|
 |
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mh. Kassim Majaliwa, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Temeke Abdallah
Diwani, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Boniface Jacob, Mstahiki Meya wa
Manispaa ya Ilala Charles Kuyeko, Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mstahiki Meya
Isaya Mwita na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
Tulia Ackson, wakati wa hafla ya utoaji madawati kwa waheshimiwa wabunge kwa
ajili ya shule zilizo kwenye majimbo yao katika viwanja vya Karemjee Jijini Dar
es Salaam.
(PICHA NA HASSAN SILAYO)
|
Na:
Lilian Lundo
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameviagiza vyombo vya
Usalama vilivyopewa jukumu la kutengeneza madawati kujipanga zaidi ili
kutekeleza kwa wakati majukumu wanayopewa.
Mhe. Rais aliitoa
kauli hiyo leo, katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kwenye hafla
ya uzinduzi wa mpango wa ugawaji wa madawati yaliyotolewa na Ofisi ya Bunge kwa
Majimbo 155 ikiwa ni awamu ya kwanza ya ugawaji wa madawati hayo.
Mnamo april 11, 2016 Mhe.
Rais alipokea hundi ya shilingi Bilioni Sita kutoka Ofisi ya Bunge na kuagiza
fedha hizo zielekezwe katika utekelezaji wa utengenezaji wa madawati ambapo Magereza
na Jeshi la kujenga Taifa (JKT) walipewa jukumu la kutengeneza madawati hayo.
Aidha Mhe. Rais amesikitishwa
na kasi ambayo JKT na Magereza wametumia katika utengenezaji wa madawati hayo,
ambapo kwa miezi mitatu wametengeneza jumla ya madawati elfu Sitini.
“Nina wasiwasi na
kasi yenu, ikiwa kwa miezi mitatu mmetengeneza madawati elfu sitini basi kuna
uwezekano wa zoezi hili la utengenezaji wa madawati mkamaliza mwaka 2017,” alifafanua
Mhe. Rais.
Aliendelea kwa kusema
kuwa, suala la madawati ni la haraka alihitaji kusubiri kwa muda mrefu hivyo vyombo
hivyo vinatakiwa kutengeneza madawati hayo kwa uharaka kwani nguvu kazi ya
kutosha wanayo.
Kwa upande wake, Naibu
Spika Mhe. Tulia Ackson amesema kuwa Ofisi ya Bunge inategemea kugawa madawati
120,000 kwa awamu mbili tofauti ambapo awamu ya kwanza imekamilika na jumla ya
madawati 61,385 yatagawiwa kwa majimbo 155 kati ya majimbo 264.
Fedha iliyotolewa na
Ofisi ya Bunge ni Fedha iliyotokana na matunda ya mpango wa Serikali wa kubana matumizi ambapo
Ofisi ya Bunge imeweza kubana matumizi na kubaki na Shilingi Bilioni Sita kwa
mwaka wa fedha 2015/2016.
No comments:
Post a Comment