KARIBU DKT.JOHN P. MAGUFULI, tuchape kazi uchaguzi
umekwisha na wananchi wameongea na sauti zao zimesikika kupitia masanduku ya
kura. Ni dhairi kuwa Dkt. John Pombe Magufuli ndiye Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa
niaba yangu binafsi na kwa niaba ya umoja wa Wazazi, Jumuiya ya CCM Mkoa wa
Morogoro tumependa kukupongeza wewe binafsi, Viongozi na wanachama wote wa
chama cha Mapinduzi kwa ushindi mkubwa
tulioupata . Ushindi huu unaonyesha kuwa wananchi wana imani na wewe lakini pia
bado wana Imani na chama
chetu cha Mapinduzi.
Lakini
kama Jumuiya tumependa pia kuwapongeza wabunge wote wa Mkoa wa Morogoro na Nchi nzima kwa ujumla kwa
kushinda na kuchaguliwa kuwawakilisha
wananchi kwenye baraza hilo muhimu la kutunga sheria. Uchaguzi umekwisha ni wakati wetu sote kumsaidia Rais
wetu kutekeleza majukumu yake bila kujali itikadi zetu kwani kama ambavyo mhe.
Rais amekuwa anasema “maendeleo
hayana vyama”.
![]() |
| Mhe.Rais,Dkt.John Pombe Magufuri akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazizi Mkoa wa Morogoro,Bi.Mecky Mdaku |
Mhe.
Rais , Sisi Wazazi Morogoro
tunakukaribisha na tunaahidi ushirikiano wetu kwako katika kusimamia
shughuli za Serikali na chama chetu. Matarajio ya Watanzania kwako ni makubwa
nasi tunaimani kuwa kwa uwezo na moyo ulionao wa kuwatumikia Watanzania na kwa
msaada wa Mungu ambaye amekuwa nguzo yako kuu utafanikiwa.
Mhe.
Rais Ilani ya chama chetu imefafanua
vizuri vipaumbele na namna ambavyo tumejipanga
kutatua kero za Watanzania na kuboresha maisha yao. Katika kipindi cha
kampeni umefanya kazi kubwa ya kuinadi
na kuifafanua Ilani yetu na huu ndio msingi wa ushindi wetu kwani tunayaamini
watanzania walikuelewa na kukuamini.
Ulipita
kila kona ya nchi hii tena kwa usafiri wa barabara jambo ambalo si tu lilikupa fursa ya kuwafikia watanzania
wengi, bali pia ulipata fursa ya kushuhudia changamoto wanazokabiliana nazo.
Tunapenda
kukupongeza wewe na timu nzima ya Kampeni akiwemo Mwenyekiti wetu wa Umoja wa
Wazazi, Jumuiya ya CCM Tanzania Abdallah M.Bulembo kwa kazi kubwa mliyoifanya.
Mhe. Rais dhamira tuliyopewa na wananchi ni
kubwa na Imani waliyoonyesha kwetu haina kipimo. Tunalo deni kwa
watanzania na kama ulivyokwisha sema
inatubidi tufanye kazi , tunapenda kukuunga mkono na kuwaomba viongozi wote
watakaoteuliwa na watanzania kwa ujumla wajiandae kuchapa kazi kwa bidii.
Uwezo
wako na dhamira yako haitiliwi shaka na mtu yeyote hivyo tunaimani kuwa ahadi
tulizowapa watanzania tutazitekeleza kwa uongozi wako. Uwezo wa kuondoa kero za
watanzania unao, uwezo wa kuongeza ajira kwa vijana unao, uwezo wa kusimamia
rasilimali za Taifa unao, uwezo wa kusimamia misingi ya haki na Amani ya nchi
yetu unao, Uwezo wa kusimamia umoja na mshikamano ndani ya chama chetu na
Serikali zake unao. Lakini kikubwa kabisa ni kuwa nia na dhamira ya dhati ya
kuwatumiakia wananchi unayo.
Kwa
mtaji huu Tanzania yenye uchumi wa kati, yenye Viwanda na uwezo wa kutumia
malighafi za ndani yenye kuboresha maisha ya wafanyakazi, wakulima na
wafugaji ndio Tanzania ya Magufuli
tunayoingojea. Ukweli ni kuwa Tanzania ya aina hii chini ya Uongozi wako inawezekana na kila
mmoja atimize wajibu wake.
Tuna
Imani kuwa Serikali unayoenda kuiunda itakuwa na sura zinazofanana na wewe
kiutendaji, itakuwa na watanzania wazalendo na wachapakazi na wenye uchungu na
Taifa lao. Tunajua utaunda Serikali ya watu wanaochukia rushwa na kubwa Zaidi
wanaochukia umaskini wa watanzania.
Kwa
upande wa chama chetu huu ni wakati wa kutathimini yote yaliyyotokea kipindi
cha kampeni. Upo ukweli kuwa baadhi ya wana CCM walishiriki kukihujumu chama
kwa njia moja au nyingine. Wapo walioshindwa kutimiza majukumu yao kwa uzembe
lakini wapo pia waliotuhujumu kwa kukusudia.
Sisi
Jumuiya ya WAZAZI Morogoro tunaamini kuwa adui wa ndani ya chama ni hatari
kuliko adui wa nje wa chama.
Tunakutakia
Afya njema na maisha marefu ili uweze kutimiza ndoto zako za kuboresha maisha ya watanzania. Karibu
Dkt. John P. Magufuli.
Kidumu chama
cha mapinduzi.

No comments:
Post a Comment