Meneja ustawi wa Jamii na Uhusiano wa Taasisi ya Tiba ya
Mifupa na Mishipa ya fahamu (MOI) Bw. Jumaa
Almasi akionesha kwa waandishi wa habari moja ya vipandikizi anavyowekewa mgojwa aliyevunjika
mfupa mrefu wa paja au chini ya goti (sign nail)ambavyo Serikali hulipia
gharama zake kutokana na gharama za vipandikizi hivyo kuwa kubwa.Kushoto ni
Afisa Uhusiano wa Taasisi hiyo Bw. Patrick Mvungi.
Meneja ustawi wa Jamii na Uhusiano wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya fahamu (MOI) Bw. Jumaa Almasi akionesha kwa waandishi wa habari moja ya skruu zinazotumika kufungia kipandikizi cha sainal kunapokuwa ndani ya mfupa. Kushoto ni Afisa Uhusiano wa Taasisi hiyo Bw. Patrick Mvungi.
Na.
Lilian Lundo- Dar es salaam.
Idadi
ya wagonjwa wa upasuaji katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu
(MOI) imeongezeka kutoka wagonjwa 20 mpaka wagonjwa 40 kwa siku.
Meneja
Ustawi wa Jamii na Uhusiano wa taasisi hiyo Jumaa Almas ameyasema hayo leo,
jijini Dar es Salaam wakati akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari juu ya tuhuma
zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa taasisi hiyo inabana matumizi na
kusababisha msongamano wa wagonjwa taasisi hiyo.
Amesema
asilimia 80% ya wagonjwa wanaotibiwa katika Taasisi hiyo wanahitaji upasuaji wa
dharura jambo ambalo limeilazimu taasisi hiyo kufungua wodi nyingine ya
upasuaji ili wagonjwa wote wanaohitaji huduma ya upasuaji wa dharura waweze
kufanyiwa ili kuokoa maisha yao.
“Msongamano
wa wagonjwa MOI hausababishwi na kubana matumizi bali ni kutokana na kuongezeka
kwa wagonjwa kutoka wagonjwa 20 mpaka wagonjwa 40 kwa siku ambapo
kumesababishwa na ongezeko kubwa la ajali hasa za pikipiki katika jiji la Dar
es Salaam,” amesema Almas.
Amefafanua
kuwa wagonjwa wa upasuaji wa kichwa na ubongo hulazimika kusubiri kwa muda kutokana
pindi wanapopelekwa katika chumba cha wagonjwa mahututi mara baada ya upusuaji
na kuongeza kuwa vyumba vya wagonjwa mahututi ni vichache ikilinganishwa na
ongezeko kubwa la wagonjwa wanaohitaji upasuaji huduma hiyo.
Amesema
taasisi hiyo inategemea kuongeza vyumba vingine zaidi kwa ajili ya wagonjwa
mahututi ili kukidhi idadi ya wagonjwa ambao wamekuwa wakiongezeka kila siku
Akifafanua
kuhusu usitishwaji wa kambi za upasuaji (surgical camps) zilizokuwa zikifanyika
siku za mapumziko amesema kuwa kambi hizo zimesitishwa kwa muda mrefu kufuatia
uamuzi wa Bodi ya wadhamini ya MOI baada ya bajeti ya kuendesha kambi hizo kuwa
kubwa ikilinganisha na mapato ambayo taasisi imekuwa ikiyapata ambayo yamekuwa yakiigharimu
Taasisi hiyo kiasi
cha shilingi milioni 5 mpaka 7 kwa wiki.
Pia
amekanusha suala la uuzwaji wa viungo
pandikizi katika Taasisi hiyo na kusisitiza kuwa sio la kweli bali Taasisi imekuwa ikipata
msaada wa vipandikizi hivyo kutoka Taasisi ya Sign Group International ya
Marekani kwa miaka mitano sasa na wagonjwa wamekuwa wakichangia gharama za
upasuaji, dawa na huduma nyingine.
Amesisitiza
kuwa Uongozi MOI unawahakikishia watanzania kwamba huduma za Taasisi hiyo zinaendelea
kama kawaida na yoyoye mwenye malalamiko juu ya huduma ya MOI afike ofisi ya
Uhusiano na Ustawi wa Jamii na malalamiko yake yatashughulikiwa.
No comments:
Post a Comment